Thursday, April 11, 2013

Namanga Sports Club yashiriki uzinduzi wa Klabu ya Msasani Jogging

Msasani Jogging wakiongoza Jogging.


Mgeni rasmi Phares Magesa akiwahutubia wanamichezo. Kulia anayechati na simu ni Mwenyekiti wa Namanga Sports Club, David Mwaka.
Klabbu ya Namanga Sports ilishiriki katika Uzunduzi wa Klabu ya Msasani Jogging uliofanyika Jumapili Aprili 07. 2013 katika Ufukwe wa Msasani jijini Dar es Salaam.

Katika hafla ya uzinduzi huo Mgeni rasmi alikuwa ni Makamu wa Rais wa Shrikisho la Mpira wa Kikapu Tanzania ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Bw. Phares Magesa.

Zaidi ya  wanamichezo 800 kutoka zaidi ya Klabu 20 vya Jogging walihudhuria akiwemo Diwani wa Kata ya Msasani (CCM), Mheshimiwa Christina Kirigiti.

Baadhi ya klabu zilizoshiriki uzinduzi huo ni pamoja Biafra, Kunduchi Kwanza, Msufini, Family Jogging, Kawe Social & Sports Club, Kawe Beach Jogging na Kunduchi Kwanza.

Klabu zingine ni pamoja na Sotojo, Ukwamani Jogging, Barafu, Mzimuni, Kata 14, Kongowe, Timberland,Unga Unga Jogging, Fanja Jogging, Dovya Jogging n.k. Habari picha kwa hisani ya Biafra Blog

No comments:

Post a Comment