Friday, March 15, 2013

Namanga Sports Club yashiriki mazoezi na Harambee ya Kunduchi Kwanza

Mnamo Machi 10, 2013 wanamichezo kutoka Namanga Sports Club, Kawe Beach, Kawe Social & Sports Club, Msasani Jogging & Sports Club, Biafra Sports Club pamoja na wenyeji Kunduchi Kwanza walikusanyika pamoja na kufanya mazoezi ya Jogging ambapo zaidi ya wanamichezo 100 walikutana pamoja na wadau wengine. Mbio hizo zilianzia Makao Makuu ya klabu ya Kunduchi Kwanza Malanja Pub iliyopo Kunduchi Mtongani kupitia Mbuyuni, Afrikana hadi round about ya Kawe na kisha kurudia njia hiyo hiyo hadi Malanja. PICHANI: Mweka Hazina wa Namanga, Michael Juma 'Mike Boss' (katikati mstari wa mbele) akiongoza mazoezi ya viungo (Aerobics). Picha kwa hisani ya Biafra Blog

Sehemu ya wakimbiaji.

Wana-Namanga pia walishiriki harambee.

Makamu Mwenyekiti wa Namanga Sports Club, Uncle Ole (kulia) na Mweka Hazina, Mike Boss wakitafakali jambo wakati wa harambee hiyo.

No comments:

Post a Comment