Friday, March 15, 2013

KIKAO CHA HARUSI YA JAMAL JOHN GAKO

Kikao cha tatu cha Harusi ya Mwanachama wa Namanga Sports Club, John Gako a.k.a JAMAL (pichani), kinatafanyika Jumapili Machi 17, 2013 katika Leecar's Pub iliyoko katika eneo la Namanga - Msasani Makangila barabara ya Kimweri jijini Dar es Salaam.

Wanamichezo toka klabu za Kunduchi Kwanza, Biafra, Namanga na vilabu vingine rafiki, wadau, wote, ndugu, jamaa na marafiki wanaombwa kuhudhuria kwa wingi ili tuweze kufanikisha Harusi ya mwanamichezo mwenzetu.

Gako anatarajia kufunga ndoa Mwishoni mwa Mwezi April.

NB: Mkija na michango ni bora zaidi, kwani muda uliobaki ni mdogo sana.

Imetolewa na:
John Badi
Mshauri wa Masuala ya Habari na Mawasiliano
Namanga Sports Club

No comments:

Post a Comment